4 Agosti 2024 - 12:28
Pakistan imeomboleza Kifo cha Kishahidi cha "Ismail Haniyeh" + video

Maelfu ya Wananchi wa Pakistan, wakiadhimisha siku ya Maombolezo ya Umma kwa Mnasaba wa kuuawa Shahidi Mkuu wa Harakati ya Hamas. Walifanya maandamano hayo kulaani vitendo vya Kigaidi vya Utawala Haram wa Kizayuni na kuonyesha Mshikamano wao kwa Taifa la Palestina.

  Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahlul_Bayt (a.s) - ABNA - Serikali ya Pakistan imetangaza rasmi leo hii kuwa Siku ya Maombolezo ya umma kufuatia kuuawa Shahidi Dkt. Ismail Haniyeh, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya vuguvugu la upinzani la Kiislamu la Hamas.

  Wakati huo huo, Miji tofauti ya Pakistan pia ilishuhudia utekelezaji wa Sala ya maiti ya bila kuwepo kwa Shahidi huyu Mujahid, na kuwepo kwa makumi ya maelfu ya wafuasi wa Palestina.

Maadhimisho ya siku ya maombolezo ya umma katika ngazi ya Kitaifa, kuidhinishwa kwa azimio la kuiunga mkono Palestina, kulaani mauaji ya Shahidi Haniyeh na vitendo vya kigaidi vya utawala ghasibu wa Israel katika Bunge la Pakistan; ni miongoni mwa matukio mengine yaliyo nchini humo hii leo.